USHUHUDA WA WALIOJARIBU KUFANYIA KAZI MAFUNZO YA KITABU CHA MILIKI KIWANDA MILIKI UCHUMI.

Habari rafiki yangu mpenda maendeleo, naamini uko vizuri na unaendelea na harakati za kuboresha maisha yako.

Leo napenda kukuletea shuhuda za baadhi ya watu ambao wamepata elimu ya utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za viwandani kupitia kwenye kitabu changu cha MILIKI KIWANDA MILIKI UCHUMI na wamefanikiwa kutengeneza products hizo na wamenitumia picha za bidhaa zao na kunipongeza kwa kuwasaidia kufikia hatua hiyo.

Picha zifuatazo ni baadhi ya picha ambazo nimetumiwa, ziangalie na wewe uhamasike kujaribu kutengeneza bidhaa yako, huwezio jua kesho unaweza kutengeneza bidhaa ikawa maarufu na ikawa ndo biashara yako na ikakutoa kimaisha

Asante sana kaka, namshukuru Mungu kupitia kitabu chako nimeweza sasa kutengeneza sabuni ya mche na ina povu jingi sana na imeanza kupendwa sana na watu wanaonizunguka. Nashukuru kwa kunisaidia kupata kazi kwani nimehangaika muda mrefu bila ajira na sasa nimepata cha kufanya naamini itanirahisishia maisha kabisa. Asante sana na Mungu akubariki.

” Kaka nimejaribu kutengeneza sabuni kulingana na maelekezo niliyoyapata kwenye kitabu chako  cha MILIKI KIWANDA na sasa nimeweza kufanya vizuri na nategemea nikirudia nitazidi kufanya vizuri zaidi. asante sana na Mungu akubariki kwa kazi yako ya kuelimisha umaa”

Kaka hii ndo kazi yangu, nimefanikiwa kutengeneza na iko vizuri sana, tatizo liko kwenye kukata sabuni, naomba usichoke kunielekeza, natamani kufanya zaidi ya hapa. Asante sana kwa msaada wako, kitabu chako kimekuwa na msaada mkubwa sana.

Kaka wewe ni mtu hatari sana, natamani watanzania wote wangeweza kujifunza kutoka kwako, umenisaidia sana na sasa ninaanza kuingia sokoni na sabuni yangu imekaa vizuri sana, Mungu akubariki sana ndugu yangu.

 

Kaka nashukuru sana kitabu chako kimenisaidia sana na sasa nimeanzakutengeneza sabuni ya Unga na imetoa povu jingi sana mpaka nimejidharau sana, kumbe mambo haya huwa yanawezekana mtu kutengeneza mwenye we nyumbani, nashukuru sana umenipatia ajira. Mungu akubariki sana Kaka.


Hizo ni baadhi ya shuhuda za watu ambao wamejaribu kufanyia kazi walichokisoma kutoka kwenye kitabu changu cha MILIKI KIWANDA MILIKI UCHUMI. 
Naamini siku si nyingi tutakuwa na watu wanamiliki viwanda vyao nyumbani kwao na watakuwa wanatengeneza pesa bila shida kabisa. Kama na wewe ungependa kujifunza ujuzi huo, basi huna budi kupata copy yako ya kitabu hiki, kitakusaidia sana na baada ya hapo tuendelee kuwasiliana ili tuweze kusaidiana pale unapokwama.
kama unapenda kupata kitabu hicho, basi BONYEZA HAPA kukipakua kitabu hicho.

Asante sana na nikutakie siku njema katika kupiga vita umaskini.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako;


PIUS JUSTUS MULIRIYE
0754745798



Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *