SAIKOLOJIA YA WATU KATIKA MITANDAO YA KIJAMII

Habari rafiki, natumai unaendelea vizuri na harakati za kukomboa maisha yako na kuelekea katika uhuru wa kifedha.

Katika mfululizo wa mada zetu juu ya jinsi ya kutumia mtandao wa internet kibiashara leo hii ninakuletea mada inayozungumzia Saikolojia ya watu walioko katika mitandao ya kijamii.

Kama tunavyojua, katika mitandao ya kijamii ni sehemu ambako watu hukutana na kujumuika pamoja, kuchati, kuonyesha style mbalimbali za maisha, kwa kulitambua hilo ninapenda kukwambia rasmi kuwa katika mitandao ya kijamii SIO MAHALI PA KUUZIA BIDHAA YAKO AU SIO MAHALI PA KUFANYIA BIASHARA YAKO.

Hii ni sawa na kuwakuta watu wako katika club wanacheza mziki na kuponda raha halafu wewe unaingia na bidhaa zako na kuanza kuwatangazia ili wanunue, nakuhakikishia watakufukuza na hata kukupiga kwa sababu unawaharibia starehe zao.

Kwa hiyo, kama wewe umekuwa ukiweka picha za bidhaa zako kila mahala kwenye mitandao ya kijamii acha mara moja tabia hiyo.

KAMA NDIO HIVYO, NINI UFANYE??

Badala ya kupost picha za bidhaa na kuwatangazia watu wanunue, tengeneza JUKWAA LAKO/KIJIWE CHAKO na huko ndiko utumie kuwaelimisha juu ya umuhimu wa bidhaa unayoitoa na kisha uwauzie, itakuwa rahisi kununua kwa sababu wameshapata elimu juu ya hiyo bidhaa kutoka kwako. Hivyo ndivo unapaswa kufanya.

JUKWAA NI NINI??
Jukwaa katika biashara ya mtandao ni sehemu maalumu ambako unatumia kuwaelimisha watu kuhusu jambo flani. Jukwaa linaweza kuwa;

  • Facebook messenger chat Bot (messenger)
  • Facebook group
  • Whatsapp group
  • Email list 
  • Youtube subscriber etc
Tumia platform hizo kukusanya watu na kisha waelimishe kisha toa ofa yako.
JINSI YA KUJENGA JUKWAA LAKO
Jukwaa linajengwa kwa kutumia software ambazo zinaruhusu watu kuweza kuingia automatically na kisha ujumbe unakuwa unawafata mara kwa mara kulingana na ulivyoset wewe.
Kama utahitaji kujua zaidi na jinsi ya kuweza kujenga na kutengeneza jukwaa lako kitaalamu nimekuandalia kozi maalumu iliyopo kwenye mfumo wa video zikielezea kwa kina hatua kwa hatua jinsi ya kuset program hizo.
Kama utakuwa tayari kujifunza zaidi ili uanze kutengeneza kipato kupitia mtandao basi jaza fomu hii chini tukishapokea fomu yako tutawasiliana na wewe moja kwa moja na tutakupa utaratibu wa kuanza kozi hiyo.

Ni mimi mwenye kujali mafanikio yako;

PIUS J. MULIRIYE
0717375782 | WHATSAPP
0754745798 | CALL | TEXT

Leave a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *